Bado haki ya Afya ya uzazi kwa wanawake na wasichana inahitajika, Waandishi waaswa kuielimisha jamii.

Waandishi wa Habari wameaswa kuongeza hamasa kwa jamii katika kuandika habari makala na vipindi mbali mbali  vinavyohusu haki ya Afya ya uzazi hususan ni kwa wanawake na wasichana  ili kuongeza usalama  wa afya zao na  kuendelea kuwa salama .

Wito huo umetolewa na Zaina Abdalla Mzee  mratibu wa mradi wa Haki ya Afya ya Uzazi kwa Wanawake na Wasichana unaotekelezwa na TAMWA_ZANZIBAR   wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wahariri katika mkutano wa tathmini juu ya  habari zinazohusu maswala ya  afya ya uzazi   uliofanyika katika ukumbi wa TAMWA _ZANZIBAR Makanjuni Pemba.

Amesema kuna wimbi kubwa la mabadiliko ya tabia kwa wasichana wakike na wakiume   ambayo huenda yasiposemewa  kupitia waandishi wa habari   afya ya uzazi kwa wasichana  ikaendelea kuwa hatarini  na kupelekea kutokufikia malengo yao ya maendeleo hivyo ni vyema kupitia  Waandishi kuitumia fursa hiyo   kuwahimiza wazazi Kuvunja ukimya kuhusu mabadiliko ya tabia sambamba na kuzunyumza na watoto wao hususan ni wasichana na wavulana katika kubadilisha tabia na mabadiliko ya kimwili ili kuwaepusha na Athari za mabadiliko ya tabia za mwili .

 kwa upande wake Ali Mbarouk Omar mwandishi mwandamizi na mkufunzi kwa waandishi wa habari katika maswala ya Afya ya uzazi amesema   kuna maswala mbali mbali yanayohusu haki ya Afya ya Uzazi bado yamekuwa yakirudisha nyuma maendeleo ya wanawake ikiwemo swala ya afya ya uzazi na maradhi yasiyopewa kipaumbele  kama vile  maradhi ya Pressure,Kisukari,Ganzi   na mengine ambayo yamekuwa  na madhara makubwa kwa jamii hususan wanawake lakini bado waandishi wamekuwa hawayasemei maswala hayo katika kazi zao za kuelimisha Jamii .

Nao baadhi  ya waandishi wa habari  waliojengewa uwezo kuhusu uwandishi wa maswala ya haki ya afya ya uzazi  akiwemo Khaulat Rashid Pamoja na Fatma Abrahman wamesema licha ya kuendelea   kuandika na kutoa taarifa kuhusu maswala mbali mbali ya Afya uzazi lakini bado ugumu wa kuwapata wataalamu wa maswala hayo kutokana na sababu mbali mbali pamoja na takwimu  mbali mbali umekuwa ukirudisha  nyuma  jitihada za waandishi hao katika kuandika habari hizo.

Kwa upande wake muhariri kutoka Radio Jamii Micheweni Rehema Ramadhan  Said Ali Masoud Kombo pamoja na  Bakar Mussa Juma  kutoka  gazeti la Zanzibar leo wamewataka  waandishi kutumia ujuzi wa kitaalamu katika kufanya ushawishi wa kupata taarifa kutoka kwa vyanzo mbali mbali sambamba na kuwasemea watendaji ikiwemo wauguzi na kuweza kupatiwa elimu  katika maswala hayo ya haki ya Afya ya uzazi .

Waandishi na Wahariri kutoka vyombo mbali mbali vya habari  wameshiriki kiatika  Mkutano huo  wa tathmini uliaondaliwa na TAMWA_ZANZIBAR  .

Post a Comment

0 Comments