Ni zama za Wanawake kushiriki kikamilifu katika Michezo mbalimbali nchini.

Imeandikwa na Tatu Juma - Zanzibar 

Chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA Zanzibar kimewataka wanawake kujitokeza kwa wingi katika kushiriki masuala ya michezo.

Wito huo umetolewa na Bi Haura Shamte alipokua akitoa mafunzo kwa wanachama wa chama hicho juu ya masuala ya michezo na uongozi kwa wanawake huko Ofisini kwao Tamwa Mkoa wa Kusini Unguja.

Amesema kuwa, kwaupande wa Zanzibar jumla ya vyama vya michezo 42 na wengi wao waliojiunga na vyama hivyo ni wanaume wakati asilimia ndogo tu niyawanawake.

Bi Haura amewataka wazazi kutokuwa na fikra potofu kwa watoto wao kwani nadharia hii inaonesha kuwa wanaume pekee ndio wanaostahiki kujihusisha katika michezo.


Hata hivyo amesema kuwa waandishi wanawake walio wengi  hawandiki habari za michezo kwa sasa ipo haja kwa waandishi pamoja na watangazaji kuchukua hatua ya kufanya utafiti na uchambuzi juu ya suala la  michezo kwa upande wa wanawake ili kufikia hatua nzuri.

Nae Mwandishi wahabari ambae pia ni mwanachama hai wa chama hicho ndugu Salma Said amesema kuwa ipo haja ya kuboreshwa kwa vyama vya michezo kwa wanawake kwa kuwekewa kanuni sahihi zisizo kiuka maadili katika jamii ili kuona wanawake wengi kujihusisha na michezo tofauti.

Wakati huohuo mwanachama mwengine wachama hicho ndugu Nasra Hatibu amesema kuwa wanawake walio wengi wanagoma kujiunga na michezo kwakuona kuwa inawezekana ukatumia muda mwingi katika kutumikia taifa pasipokuwa na maslahi mazuri yakifedha hivyo ipo haja ya kufanyiwa utatuzi tatizo hilo ili jamii iweze kuona mafanikio hatimae kujitokeza kwa wingi.

Post a Comment

0 Comments