TAMWA-ZNZ YATOA ELIMU KWA SEKTA YA USAFIRISHAJI KUHUSU MAPAMBANO DHIDI YA UDHALILISHAJI WA KIJINSIA.

Imeandikwa na Tatu Juma - Zanzibar 

Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Zanzibar (TAMWA-ZNZ) kimetoa mafunzo maalum ya siku moja kwa watoa huduma za usafirishaji wa umma kutoka Wilaya ya Kaskazini A, Unguja, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha mapambano dhidi ya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia katika sekta ya usafirishaji visiwani Zanzibar.

Mafunzo hayo yamewakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo waendesha bodaboda, , madereva wa magari ya abiria, madereva wa bajaji, askari wa usalama barabarani pamoja na Afisa Takwimu kutoka Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

 Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uelewa na kuwashirikisha watoa huduma wa usafiri usio rasmi katika kuzuia na kupambana na vitendo vya ukatili na udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto wa kike, pamoja na kuhakikisha wanawake na wasichana wanapata huduma za usafiri katika mazingira salama na yenye heshima.

 Akizungumza katika mafunzo hayo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Mkokotoni, Afisa Programu kutoka TAMWA-ZNZ, Asia Hakim Makame, amesema mafunzo hayo yataongeza uwajibikaji kwa watoa huduma za usafiri, kubadili mitazamo hasi kuhusu wanawake na kusaidia kuifanya sekta ya usafiri kuwa sehemu salama kwa wanawake wanaotumia usafiri huo na jamii.

Post a Comment

0 Comments