"NAMNA YA KUWAKIRIMU MAYATIMA NI HIVYI , SOTE TUWE HADIDHI NJEMA YA KUSIMULIWA"

NA-MWANDISHI WETU 
Club ya Mazoezi ya Viungo Gombani Fitness imewajumuisha pamoja watoto mayatima 15 wananchama Wasiopungua 60  wa Club hiyo ,na vilabu vyengine maeneo  mbali mbali kusini Na kaskazini Pemba  Katika Iftaar Maalum iliyofanyika Katika Ukumbi wa ZRA Gombani Chake Chake ikiwa ni muendelezo   na utaratibu unaofanywa na Club hiyo kila Mwaka.
Akizungumza mara baada ya ghafla ya iftar hiyo Afisa Mdhamini Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Ahmed Abuubakar  amewataka wana Club hiyo kuongeza bidii kuwafutarisha mayatima na wasiojiweza   waliozunguka mitaani na katika jamii  ili kuweza kujumuika nao pamoja   ili mkusanyiko huo uweze kupata  fadhila na ujira mkubwa Zaidi.
Amesema Fadhila na Hikma  katika michanganyiko ya hairat inaweza kuongezeka mara dufu iwapo walengwa wakiwemo mayatima na wasiojiweza wataongezeka katika mkusanyiko huo mwaka ujao..
Aidha ameipongeza Gombani Fitness  kwa  kuona umuhimu wa kuftarisha ambapo pia ametumia fursa ya mkusanyiko huo kuwataka wananchi na vijana kuendelea Kudumisha amani iliyopo hususan kuelekea Uchaguzi.

Ahmed pia aliwataka wananchi kisiwani Pemba kuepuka kuwasema  vibaya viongozi bila kuwafika wahusika yanapojitokeza matatizo mbali mbali ili waweze  kuisaidiaPemba  kwa pamoja kuzipatia ufumbuzi changamoto mbali mbali.

Hata hivyo amewaasa wananchi kisiwani humo Kuyatumia Majengo  ya Serikali kama majengo  ya kuzipatia  ufumbuzi changamoto jamii  na siyo kuyaogopa wanapopatwa na changamoto.

Aidha amewaasa Gombani fitness kuwashirikisha mapema katika mambo ya Hairat yanapojitokeza ili nguvu na mchango wa serikali uweze kuingia katika heri hizo.

 Nae     Mwenyekiti wa Club Hiyo Hamad Malengo  amewaasa  waumini wengine kuiga utaratibu huo ambao hauhitaji  uwezo mkubwa kutimiza sunna hiyo ya kufutarisha watu mbali mbali.
Aidha amewakumbusha kuzisdisha bidii kufanya ibada  zaidi katika mwezi huu wa Ramadhan.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo amewataka Wananchi na waalikwa hao kujiunga katika vikundi vya mazoezi ili  kuimarisha Afya na miili yao.

Post a Comment

0 Comments