Wizara ya Kilimo na wizara ya Biashara watakiwa kushirikiana kwa kulilinda na kulithamini zao la karafuu

Waziri wa  Kilimo Umwagiliaji na Mifugo Zanzibar Mhe, Shamata Shaame Khamis amesema, Wakulima, wizara ya Biashara na Wizara ya Kilimo wanawajibu wa  kushirikiana na kuhakikisha wanalilinda na kulithamini zao la karafuu na kuendelea na upandaji miche hiyo hasa katika kipindi hiki cha mvua za masika zinazoendelea.
Akizungumza  leo katika Uzinduzi wa Ugawaji wa miche  ya mikarafuu Tangaani Mkoa wa Kusini Pemba katika hafla iliyoandaliwa na Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) kwa mashirikiano na wizara hiyo Amesema kuwa wananchi wana dhima ya kuendeleza na kulinda karafuu ya Zanzibar kwani ndio uti wa mgongo wa uchumi wa nchi, hivyo Serikali kupitia wizara ya kilimo na Shirika la Biashara litaendelea kununua miche hiyo na kuitoa kwa wananchi bure ili kuweza kuendeleza zao hilo na kuleta tija kwa wananchi.
Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC). Nd, Soud Said Ali  amesema  kuwa Juhudi  kubwa inayochukuliwa na Shirika la biashara  kwa kushirikiana  na wizara ya kilimo katika kuhakikisha linaendelea kuzalisha miche ya mikarafuu na kuitoa kwa wananchi ili kuongeza kasi ya  uzalishaji wazao hilo ni chachu ya maendeleo na ukuwaji wa  zao la karafuu nchini. 
Aidha amesema kwasasa Shirika kwa kushirikana na wizara ya Kilimo limeandaa utaratibu maalum wa kufatilia miche yote inayotolewa ili kujua maendeleo ya  ukuwaji ya miche hiyo kwa ustawi wa taifa.

Kwa Upande wake Katibu Mkuu wizara ya Kilimo Umwagiliaji na Mifugo Nd, Ali Khamis Juma. Ameeleza kuwa mpango wa utoawaji wa miche ya mikarafuu ukiendelezwa na wananchi utaleta tija kwa taifa na kuongeza uzalishaji wa zao la karafuu nchini.

Nao wananchi waliokabidhiwa ,miche hiyo wameushukuru uongozi wa Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC). kwa mikakati wanayoichukua katika uzalishaji na utowaji wa miche ya Mikrafuu kwa wananchi bila ya malipo ili kendelea kuongeza uzalishaji wa zao hilo.

Post a Comment

0 Comments