NA-ARAFA ABASS PEMBA
UONGOZI WA wa Shehia ya Dodo,Pujini Wilaya ya Mkoani mkoa Kusibi Pemba
Umewataka wananchi wa shehia hiyo kuendelea kudumisha Amani iliyopo na kuepukana na vishawishi vitakavyopelekea uvunjifu wa amani na kupelekea madhara kwa wananchi.
Wito huo umetolewa na Ridhiwani Assa Omar sheha wa Shehia hiyo ya Dodo pujini alipikuwa akizungumza na wananchi Katika mkutanowake maalum na wananchi ndani ya shehia hiyo wenye lengo kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa amani kuelekea Uchaguzi mkuu 0ctobar 29 mwaka huu.
Akmesisitiza kuwa uongozi wa shehia hiyo hautokubali kuona mwananchi yeyote anavuruga amani katika shehia hiyi kwani madhara yake ni makubwa zaidi iwapo itatokea kutetereka na waathirika wakubwa zaidi ni wanawake watoto pamoja n na wazee.
Sheha Ridhwan amewataka wazazi na walezi kuwaelekeza vijana wao kutokaa makundi makundi kwani itapeleka kuzungumza maneno yasiyo na msingi nakupelekea kushiriki katika vitendo vya uvunjifu wa amani .
" baadhi ya Makundi makundi ambayo yamekuwa wakikaa vijana tayari yameanza kuonesha ishara mbaya ikiwemo kulenga mawe,na kutoa maneno ya kashfa kwa magari ya vyombo vya ulinzi na usalama na wakishafanya hivyo hukimbilia mabondeni hii siyo ishara nzuri kwaio naomba wazazi nao muendelee kuwakanya watoto hususan ni vijana kuacha mara moja tabia hizo ili kuendelea kutawala amani katika shehia hiyo.
Kwa upande wake Afisa Mkaguzi wa Shehia ya Dodo Ali Juma Abdulla amesema kuwa Jeshi la Polisi limejipanga kikamilifu kukabiliana na aina yoyote ya vurugu na tayari limejikita katika kulinda amani na wala sio kuwatisha wananchi .
" kwakupiga doria Maeneo mbali mbali sisi jeshi la polisi tayari tumeshajipanga lengo za hizo doria ni kuhakikisha amani na usalama unakuwepo wakati huu kuelekea uchaguzi ndani na hata baada ya uchaguzi kwahiyo wananchi wajibu wenu ni amani tuendelee kuidumisha ba hifu ya doria za Askari.
Aidha Mkaguzi huyo ametoa wito kwa jamii kushirikiana na viongozi wa shehia na jeshi la polisi kuripoti dalili zozote za uvunjifu wa amani ili hatua zichukuliwe mapema kabla amani haijatoeka na kupelekea madhara kwa wananchi na taifa.
0 Comments