Imeandikwa na Maryam Nassor - Zanzibar
WAANDISHI wa Habari nchini wametakiwa kujihakikishia ulinzi na Usalama wao kwanza kuelekea kipindi cha uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.
Wito huo,
umetolewa August 6, 2025 huko katika Afisi za TAMWA ZNZ Tunguu , na
mkufunzi wa Mafunzo ya ulinzi na usalama kwa waandishi wa Habari wa Unguja
Maryam Nassor akimuwakilisha ToT Najjat
Omar kutoka klabu ya wandishi wa Habari Zanzibar ( ZPC).
Amesema , ulinzi na usalama wa mwandishi wa
Habari unaanza na yeye mwenyewe hivyo ni lazima kujihakikishia
ulinzi na usalama , huku wakizingatia kunaelekea katika kipindi cha uchaguzi mkuu ambacho ni
hatarishi kwa wandishi wa Habari.
“ Waandishi
lazima muwe makini katika kipindi hichi tunachoelekea kwani musipokuwa makini
munaweza kuingia kwenye matatizo na kuhatarisha maisha yenu “ amesema mkufunzi huyo.
Aidha
amewataka wandishi wa Habari kujilinda
pia katika mitandao ya kijamii na kujiepusha kufungua viunganishi ( links) ambavyo
sio salama na hawajui vinapotoka.
Amesema kuwa, ni
vyema wandishi wa Habari kulinda taarifa zao binafsi zisifike kwa watu wasiohusika ili kuzuwia udukuzi na wizi wa taarifa.
Nao baadhi ya wandishi waliyobahatika kupata
mafunzo hayo, Jesse Mikofu kutoka gazeti
la mwananchi Zanzibar ameshauri ni vyema elimu kama hiyo kupewa na wamiliki wa
vyombo vya Habari ili kusaidia kuwapatia vitendea kazi ambavyo vitasaidia
kuwalinda.
Amesema kuwa, vyombo vingi vya Habari
hawahamasishi waandishi wao, kuwa na vifaa vya kujilinda kama Press Jacket na vyenginevyo wakati wa majanga.
Nae, mshiriki Samira Abdalla kutoka online ya ZU, ameshukuru kupatiwa mafunzo
hayo ya ulinzi na usalama hasa kuelekea kipindi hichi cha uchaguzi, na
kuahidi kuyafanyia kazi.
Mafunzo hayo ya siku mbili kwa waandishi wa Habari yanalenga kumasisha ulinzi na usalama kwa wandishi wa Habari
kuelekea kipindi cha uchaguzi.
mwisho
0 Comments