WANUFAIKA mradi wa SWIL Kisiwani Pemba wamepongeza mashirikiano mema yanayoendelea kufanywa na ubalozi wa Norway, nchini Tanzania katika kutatua changamoto zinazowakabili wanawake ili kuweza kuufikia usawa wa kijinsia na kuweza kushiriki katika nafasi za Uongozi ngazi mbalimbali.
Wakitoa pongezi hizo kwa nyakati tofauti katika mkutano uliofanyika katika ofisi za TAMWA kwa upande wa Pemba wanufaika hao wakiwemo,wanawake wagombea vyama mbalimbali, waandishi na, wahariri vyombo mbalimbali vya habari,wananchi maeneo tofauti, walionufaika kupitia ufadhili wa Norway nchini Tanzania ambao wanaendelea kufadhili mradi wa kuwawezesha wanawake kuwa viongozi SWIL unaotekelezwa na TAMWA ZNZ ,PEGAO, JUWAUZA na ZAFELA.
Wamesema mradi huo wa SWIL chini ya ufadhil wa Norway Tanzania umegusa jamii moja kwa moja hususan ni wanawake katika kuzipatia ufumbuzi changamoto zilizokuwa zinawakabili katika kufikia ndoto zao za kushiriki katika uongozi.
Akisimulia mabadiliko aliyoyapta kupitia mradi huo Katija Mbarouk Ali ,amesema awali alikosa utayari katika kushiriki katika mchakato wa kutafuta nafasi ya uongozi hususan katika majimbo ,lakini kupitia mradi huo aliweza kujitolea ,kujiamini na kuongeza uthubutu kuwania nafasi hiyo licha ya kushindwa kutokana na sababu zilizopo katika michakato ndani ya vyama pamoja ,na mitazamo ya wanajamii.
Wakiwa katika mkutano wakutoa ushuhuda akiwemo Halima Suleiman Kombo, Hasina Omar Salim, Tatu Abdalla Msellem na Maryam Hemed Said wameuomba ubalozi wa Norway kuendelea kuwaunga tena mkono ili kufanya kazi kubwa Zaidi ya kuwasaidia wanawake kufikia nafasi za Uongozi.
Kwa upande wandishi na wahariri wa vyombo vya habari kutoka gazeti la Zanzibar leo kisiwani Pemba Radio jamii Mkoani pamoja na radio jamii Micheweni akiwemo Ali Massoud kombo,Bakar Mussa Juma, pamoja na Amina Massoud Jabir wamesema elimu iliyoitolewa kupitia mradi huo wamenufaika katika kuisaidia jamii kuthamini mchango wa wanawake ,kuandika habari zenye kuitetea jamii ya wanawake,kuanzisha madawati ya kijinsia katika vyombo vyao,kubadilika nafasi za juu za uongozi katika vyombo vyaom kupata vitendea kazi pamoja na fedha .
Awali akizngumza na wanufaika hao Balozi wa Norway nchini Tanzania Tone Tinnes amewataka watekelezaji wa mradi huo wa SWIL kisiwani pemba ambao ni TAMWA ZNZ pamoja na PEGAO ,kuendeleza juhudi hizo za kuwasaidia wanawake katika kufikia usawa wa kijinsia bila kukata tamaa kutokana na changamoto zinzorudisha nyuma ,kwani juhudi za kuufikia usawa huo zinahitaji uvumilivu .
Ameongeza kuwa ili kuweza kuufikia utajiri wa usawa wa kijinsia kama uliofikiwa na nchi ya Norway ni lazima kuendeleza juhudi hizo bila kukatishwa tamaa na changamoto zinazojitokeza katika maeneo mbali mbali.
Kwa nyakati tofauti mkurugenzi wa TAMWA ZNZ Mzuri Issa Ali amewashukuru wanufaika hao katika kuendeleza mashirikiano mema ya utekelezaji wa mradi ,ambapo amewaasa kuendeleza mashirikiano hayo ili kuweza kuufikia usawa wa kijinsia .
Ziara hiyo maalum ya siku tatu kutoka kwa ubalozi wa Norway Tanzania kuonana kuzungumza na wanufaika wa mradi wa SWIL unguja na Pemba nchini,ilianza katika kisiwa cha Unguja ikiwa ni ufuatiliaji wa mradi wa SWIL.
MWISHO.
0 Comments